Habari na Matukio WhatsApp
Careers & Opportunities

Nafasi za Kazi Manispaa ya Morogoro 03-06-2025

Nafasi za Kazi Manispaa ya Morogoro 03-06-2025

Nafasi za Kazi Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imepokea kibali cha ajira mpya kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Kibali hiki kina Kumb. Na. FA.97/288/01/A/25 cha tarehe 29/04/2025 pamoja na kibali cha ajira mbadala Kumb. Na. FA.228/613/01G/049 cha tarehe 14/04/2025.

Watanzania wote wenye sifa wanakaribishwa kutuma maombi kwa nafasi zifuatazo:

1. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 11

Majukumu ya Kazi

  • Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kuhakikisha usalama.
  • Kuwasafirisha watumishi katika safari za kikazi.
  • Kufanya matengenezo madogo ya gari.
  • Kuweka kumbukumbu za safari katika log book.
  • Kusambaza nyaraka mbalimbali.
  • Kufanya usafi wa gari.
  • Kufanya kazi nyingine utakazoelekezwa na msimamizi wako.

Sifa za Muombaji

  • Awe na cheti cha kidato cha nne (Form IV).
  • Awe na leseni ya daraja C au E.
  • Awe na uzoefu wa kuendesha kwa angalau mwaka 1 bila kusababisha ajali.
  • Awe amehitimu mafunzo ya msingi ya uendeshaji magari kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Ngazi ya Mshahara:

TGS B (Mishahara ya Serikali)

2. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 4

Majukumu ya Kazi

  • Kuorodhesha barua zinazoingia na zinazotoka.
  • Kusambaza majalada kwa watendaji na kuyapokea yanaporudi.
  • Kuhifadhi majalada kwenye shabaka au kabati maalum.
  • Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani ya taasisi.

Sifa za Muombaji

  • Cheti cha Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
  • Awe na Stashahada (NTA level 6) ya Utunzaji Kumbukumbu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
  • Awe na ujuzi wa kutumia Kompyuta.

Ngazi ya Mshahara:

TGS C (Mishahara ya Serikali)

MASHARTI YA JUMLA

  1. Waombaji wote ni lazima wawe Raia wa Tanzania wenye umri kati ya miaka 18 hadi 45.
  2. Waambatishe:
    • CV yenye maelezo ya kutosha, anwani, namba za simu, na barua pepe inayofanya kazi.
    • Majina ya wadhamini watatu wa kuaminika.
    • Nakala za vyeti vya elimu na taaluma vilivyothibitishwa na wakili/mwanasheria.
  3. Hati za matokeo (slips), Testmonials, Provisional results hazitakubalika.
  4. Waombaji waliomaliza masomo nje ya nchi wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU/NECTA/NACTE.
  5. Wastaafu wa utumishi wa umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kwa kibali rasmi kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi.
  6. Taarifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria.
  7. Mwisho wa kutuma maombi: 11 Juni 2025.
  8. Maombi lazima yaambatane na barua ya maombi iliyosainiwa na ipelekwe kwa:

Mkurugenzi
Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro
S.L.P 166
MOROGORO

  1. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa kielektroniki wa ajira (Recruitment Portal) https://portal.ajira.go.tz

Maombi yasiyowasilishwa kwa mfumo huu hayatazingatiwa.

Pakua PDF hapa

Leave a Comment